ERIC WAINAINA LYRICS

"Fungeni Macho"
(feat. MC Kah)

Verse 1

Tulifunga macho kuomba
Tuliibiwa ardhi
Bendera ya Mungu ilipeperuka
Mwafrika akikaa kwa imani
Cheupe kilijiuza
Cheusi kilifukuzwa
Tuliambiwa,˜Imbeni alleluia.
Fungeni macho imbeni.

Chorus

Tumegongwa tumeamka
Tumekanyagwa tumejitoa
Tumelazwa tumesimama heye!
Tumebanwa tumeepuka
Kusulubiwa tumeshuka
Tumeuawa tumefufuka aye!

Verse 2

Mwaka wa 1963
Tulijishindia Uhuru
Bendera ya Mzungu iliteremshwa
Mwafrika alianza kujitawala
Tuliambiwa, ˜Harambee! Harambee!
Furuteni mzigo.
Tuliambiwa Fuata Nyayo!
Fungeni macho fuata Nyayo!

Chorus

Tumegongwa tumeamka
Tumekanyagwa tumejitoa
Tumelazwa tumesimama heye!
Tumebanwa tumeepuka
Kusulubiwa tumeshuka
Tumeuawa tumefufuka aye!


Verse 3

Na bado twangoja wokovu
Twangalia milimani
Twauliza mwokozi ni nani
Twafaa kutazama kiooni
Kila mmoja ni kiongozi
Kila mmoja ni mwalimu
Kila mmoja ni mjenzi
Kila mmoja achukue madaraka

[www.mistari.com]
All lyrics are property and copyright of their owners. All lyrics provided for educational purposes only.
Copyright © mistari.com 2009