JAMNAZI AFRICA LYRICS

"Riziki"

Mimi ninalo jambo

la nisumbua akili
ulimwengu umepasuka mahali

mungu aliupanga usiku saa ya kulala

mbona walimwengu mmebadili mipango ?
Usiku sasa imegeuka mchana
na mchana sasa ni kama usiku – jamani – yeaa eah

mi – nashangaa yeaa

repeat

karo za watoto mnatafuta usiku
kodi za nyumba mnatafuta usiku
biashara nyingi mnafanya usiku
chai kwa mkate sasa mnauza usiku
mahindi choma sasa mnauza usiku
malimali sasa mnauza usiku
hata maombi nyingi mnafanya usiku

koinange mnatafuta usiku
wake kwa waume shughuli zenu usiku
hata safari nyingi mnaenda usiku
biashara zote mnafanya usiku
kwa nini? yeaa eah

mi – nashangaa

repeat

niliambiwa na babu yangu
kweli
zubaazubaa
utapata mwana si wako

2x

nimeamini kilichosemwa na babu
nimekubali kilichosemwa na babu

Mgaagaa na upwa hali wali mkavu

lakini sasa mwapumzika saa ngapi ?
Asubuhi mnatafuta riziki
mchana kutwa mnatafuta riziki
hata majioni mnatafuta riziki
usiku wa manane mnatafuta riziki
mnabieni mnapumzika saa ngapi wenzangu

mi – nashangaa

niliambiwa na babu yangu
kweli
zubaazubaa
utapata mwana si wako

repeat

[www.mistari.com]
All lyrics are property and copyright of their owners. All lyrics provided for educational purposes only.
Copyright © mistari.com 2009